Powered By Blogger

Thursday, March 22, 2012

VIJEMBE KIKWELIKWELI


"Wenzetu alama yao ni kama kijiti hiki mnavyokiona!, achaneni nacho kitupeni, mpigieni kura Sioi alete maendeleo Arumeru." akasema Elirehema Kaaya ambaye naye 'alikula sahani moja' na Sioikwenye kura za maoni za CCM. Kushoto ni mratibu wa kampeni za CCM kitaifa Mwigulu

Nchemba akijibu tuhuma za chadema

Akizungumzia kuhusu CHADEMA kulalamikia Tume ya Uchaguzi kuwa haitawatendea haki kwenye uchaguzi huo, Mwigulu alisema, hata safu yao ya uonozi tangu Mwekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe hadi wabunge ikishika nafasi zote kwenye Tume hiyo CCM lazima itashinda uchaguzi wa Arumeru Mashariki utakaofanyika Aprili Mosi mwaka huu.
"Kwa Uchaguzi huu wa Arumeru Mashariki, hata Katibu Mkuu wa CHADEMA Dk. Wilborod Slaa awe Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Mbowe (Mweyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe) awe Mkurugenzi wa Uchaguzi, Zitto (Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Kabwe Zitto) awe Msimamizi Mkuu wa Uchaguzi  na wabunge wote  wa CHADEMA  wawe wasimamizi wa uchaguzi huo, halafu CCM tuweke mawakala tu, naapa kikwetu CCM itashinda", alisema Mwigulu.

Alisema malalamiko ya CHADEMA dhidi ya vyombo vitakavyosimamia uchaguzi huo ni woga wa kushindwa kwa sababu wanafahamu kuwa CCM imejiimarisha vya kutosha Arumeru Mashariki na italirejesha jimbo. 

No comments:

Post a Comment