Powered By Blogger

Saturday, November 10, 2012

Rukwa wawajia juu wanaobeza safari za Rais Kikwete nje

Posted on May 28, 2009 by admin
Wana-Rukwa: Wanaodai Rais Kikwete
anasafiri sana wameishiwa hoja
. Mkoa huo wasema kuwa hao ni watu wa kupuuzwa tu
. Wasema kuwa safari za Rais zimeuwezesha mkoa kupata barabara ya kwanza kubwa ya lami

Na Mwandishi Maalum
MKOA wa Rukwa umewalaani watu wanaosambaza madai kuwa safari za Rais Jakaya Kikwete nje ya nchi hazina faida na kuwa amekuwa anatumia muda wake mwingi nje ya nchi badala ya kushughulikia matatizo ya ndani.
“Tunawalaani kabisa wanaosema kuwa ukienda nje unapoteza wakati,” imesema sehemu ya taarifa ya Mkoa wa Rukwa iliyotolewa na wana-Rukwa usiku wa jana, Jumatano, Mei 27, 2009, kwenye Hoteli ya Kilimanjaro-Kempiski mjini Dar Es Salaam.
Wana-Rukwa walieleza msimamo wao huo katika hotuba ya shukurani iliyosomwa na Mwenyekiti wa CCM wa mkoa huo, Hypolite Matete katika hafla kubwa ya uchangiaji elimu katika mkoa huo.
Kiasi kikubwa cha jumla ya sh bilioni 1.9 zilichangwa ama kuahidiwa katika hafla hiyo ambako Rais Kikwete alikuwa mgeni rasmi na alisaidia katika kunadi baadhi ya vitu, ili kutunisha mfuko huo wa elimu wa mkoa huo, unaojulikana kama Mfuko wa Elimu wa Mwalimu Nyerere.
Akiwashukuru waliochangia harambee hiyo, Mwenyekiti Matete alimwambia Rais Kikwete kuwa mkoa wa Rukwa unawaalani wote wanaodai kuwa safari zake za nje hazijailetea Tanzania manufaa.
Matete alisema kuwa bila safari za namna hiyo na uhusiano wa karibu wa Rais Kikwete na aliyekuwa kiongozi wa Marekani, Rais George W Bush wala Tanzania isingepata fedha za ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilomita 230 kwa kiwango cha lami kutoka Tunduma hadi Sumbawanga chini ya msaada wa Serikali ya Marekani kupitia shirika lake la MCC.
“Tunakushukuru Mheshimiwa Rais kwa kuuwezesha Mkoa wa Rukwa kuunganishwa kwa barabara ya kwanza muhimu ya lami na mkoa mwingine. Tunakushukuru kwa kuendeleza kilimo na kuinua kipato cha wakulima katika Mkoa wa Rukwa,” alisema Matete na kuongeza:
“Kwa sababu ya upatikanaji wa mbolea, mbegu bora kwa wakati, na mpango wa Stakabadhi Ghalani kipato cha wakulima wetu kimeongezeka. Ni kilimo tu kinachoweza kubadilisha maisha ya watu wetu kwa sababu asilimia 80 ya Watanzania wanaishi kwa kutegemea kilimo. Sasa tunaamini fika kuwa dhamira ya Serikali yako ya maisha bora kwa kila Mtanzania itatekelezwa.”
Mwenyekiti huyo alisema: “Watu wanaosema kuwa unazurura kwa kutafuta wawekezaji wa kuja kuinua uchumi wa Tanzania ni watu wameishiwa hoja. Tusisumbuke nao. Endelea kuhangaika kwa sababu maendeleo hayana mwisho.”
Mwenyekiti huyo alikuwa anatoa shukurani kufuatia hotuba ya Rais Kikwete ambaye mbali na kuelezea maendeleo ya ujenzi wa barabara ya Tunduma hadi Sumbawanga, pia alielezea jitihada za Serikali yake katika ujenzi wa barabara nyingine za mkoa wa Rukwa.
Alisema Rais Kikwete katika hotuba yake: “Nafurahi kusema kwamba jitihada za ujenzi wa barabara ya lami ya kilomita 230 kutoka Tunduma hadi Sumbawanga ni ajenda yetu kuu. Tumehangaika nayo siku nyingi lakini sasa mchakato wa kuanza ujenzi unaendelea vizuri…Nimeahidiwa kuwa zabuni zitakuwa tayari Agosti ama Septemba 2009, na kazi ya ujenzi inatarajiwa kuanza mwishoni mwa mwaka huu au mwanzoni mwa mwaka jana.”
Aliongeza Rais Kikwete: “Kwa barabara za ndani ya mkoa, tunayo misaada kutoka Benki ya Dunia kwa ajili ya ukarabati na uimarishaji wa barabara ya kilomita 230 kutoka Sumbawanga hadi Mpanda, na barabara ya kilomita 87 kutoka Chala mpaka Katongoro hadi Kilando.”
Aliongeza: “Serikali ya Denmark nayo imekubali kusaidia ujenzi wa kilometa 148 za barabara kutoka Kilyamatundu hadi Muze. Mpango wa upanuzi wa bandari ya Kasanga katika Ziwa Tanganyika unafanywa na Mamlaka ya Bandari.”
“Lakini bado watu wengine wanatuambia tunazurura tu,” alisema Rais bila kuingia katika undani wa kauli yake hiyo.
Hata hivyo, watu wachache pamoja gazeti moja la Mwananchi jana na leo limeandika habari za kuonyesha kuwa ziara za Rais nje ya nchi hazina faida na kuwa Rais Kikwete anatumia muda mwingi nje ya nchi.
Mwananchi limeandika habari hiyo jana likikariri makala iliyochapishwa katika jarida la Economist la Mei 7.
Pamoja na Mwananchi kuandika habari hiyo siku 20 tokea ziandikwe kwenye jarida hilo, halikuchapisha undani wa kweli kweli wa makala hiyo uliokuwa unasifia mafanikio ya Serikali ya Rais Kikwete katika masuala mengine.
Makala ya awali ya Economist inasisitiza kuwa kutokana na mafanikio hayo ya utendaji wa Serikali ya Rais Kikwete, hakuna shaka kuwa Rais huyo atachaguliwa tena kwa kishindo katika uchaguzi mkuu wa mwaka ujao.
Shutuma hizo za Rais kusafiri nje, zimekuwa zinatolewa kila mara Rais Kikwete anapokuwa na safari za Marekani na wala siyo kuhusu safari nyingine.
Wakati wa safari ya juzi ya Marekani, Rais Kikwete, miongoni mwa mambo mengine alikuwa kiongozi wa kwanza wa Afrika kukutana na Rais Barack Obama tokea kiongozi mpya wa Marekani kupata madaraka ya kuongoza Marekani.
Katika mkutano huo, Rais Obama amehakikishia Rais Kikwete kuwa Marekani itaendeleza mipango yake yote ya misaada kwa Tanzania

NAPE aikomalia chadema

NAPE AIKOMALIA CHADEMA.
by Chama Cha Mapinduzi (CCM) on Tuesday, August 28, 2012 at 7:44am ·
L Akataa kuomba radhi, asema tuhuma atazithibitisha mahakamani
L Amtaka Dk. Slaa kuandaa bilioni 3 na shilingi moja
L Ni kwa kudai CCM inaingiza siala nchini.
NA MWANDISHI WETU
KATIBU wa Halmashauri Kuu ya Taifa Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye amewataka Chadema kwenda mahakamani haraka badala ya kusubiri kuombwa radhi kama walivyotaka ili kusafishwa dhidi ya madai ya chama chao kupewa mabilioni ya fedha na mataifa tajiri.
Aidha amemtaka Katibu Mkuu wa chama hicho Dk. Wilbrod Slaa kuiomba radhi CCM la sivyo itamburuza mahakamani kudai fidia ya sh. bilioni 3 na shilingi moja, kwa kuituhumu uongo kwamba imeingiza silaha kutoka nje ya nchi tena bila kulipia ushuru.
Nape alisema hayo leo Agosti 27, 2012, kweneye mkutano wake na waandishi wa habari, uliofanyika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, mtaa wa Lumumba mjini Dar es Salaam.
"Bila shaka mmesikia jana Chadema wakinitaka niombe radhi au wananipeleka mahakamani kudai fidia ya sh. bilioni 3, kwa madai eti nimesema Chama hicho kinapata mabilioni ya fedha kutoka kwa mataifa tajiri. Mkubwa hatishiwi nyau, nawataka waende haraka mahakamani wala wasisubiri hizo siku saba", alisema Nape.
Alisema, CCM inao ushahidi wa kutosha kuhusu madai aliyotoa Nape dhidi ya Chadema na kwamba huyo tayari kutoa uthibitisho huo mahakamani badala ya kuomba radhi.
"Nadhani wakienda mahakani itapendeza zaidi maana huko ndiko pazuri kutoa uthibitisho kuhusu tuliyosema, na ninawahakikishieni tukishathibitisha na Msajili wa Vyama akaupata uthibitisho huo chama chao kinafutwa", alisema.
Kuhusu CCM kumburuza Dk. Slaa mahakamani, Nape alisema, ameshawaagiza wanasheria wa Chama, kuandaa barua ya kusudio la mashitaka hayo, na Dk. Slaa atapelekewa ili aamue kama ataomba radhi au atakuwa tayari kwenda mahakamani.
"Wakati wanakwenda mahakamani, Chadema wamwambie babu yao ajiandae kuomba radhi au kuburuzwa mahakamani kuilipa CCM fidia ya sh. bilioni 3 na shilingi moja kwa kuizushia CCM uongo kwamba inaingiza silaha nchini tena", alisema Nape.

Thursday, March 22, 2012

JIHADHARI NA PROPAGANDA


WEDNESDAY, MARCH 21, 2012

MAJIMAREFU AWAKA KUUNGANISHWA NA NASSARI WA CHADEMA KATIKA PICHA ANAYODAI NI FEKI

'Picha hii nilipigwa nikiwa na huyu mbunge mwenzangu, Vicent Nyerere (kulia), lakini huyu wa kushoto (Joshua Nassari) hakuwepo karibu yangu kabisa! Yeye alikuwa mbali akiamrisha vijana wanichome moto tena akiwa na hasira, tofauti na anavyocheka katika picha hii. Huu ni mchezo mchafu wa kuunganisha picha kwenye kompyuta uliofanywa na CHADEMA na kwa makusudi gazeti hili likaichapisha, baada ya kuona kwamba hatua aliyofanya Nassari ya kutaka niuawe jana ni mbaya sana. Nitalishitaki gazeti hili". Analalamika Mbunge wa Korogwe Vijijini Stephen Ngonyani wakati akionyesha picha inayomuonyesha akiwa katika furaha ya hali ya juu yeye, Nyerere na Nassari. Picha hiyo imechapishwa leo ukurasa wa kwanza gazeti la Mwananchi.
Picha yenyewe anayolalamikia Profesa Majimarefu ndiyo hii kama tulivyojaribu kuinakili kutoka gazeti la mwananchi. Mdau hebu itazame kwa makini, je ni halisi au feki,  hasa ukitazama vizuri kwenye kwapa la Nassari lililokutana na Ngonyani? Pia tunamkaribisha mpigapicha wa picha hii, Edwin Mjwahuzi kama hatajali atupe picha 'orijino' ya hii tuliyonakili kwa ajili ya kuthibitisha ukweli.

Nukuu iliyojaa hekima
"Mtu mzima mwenye akili timamu akakushauri upuuzi ilhali anafahamu wazi kuwa wewe pia unazo akili timamu ukiukubali upuuzi wake atakudharau"

VIJEMBE KIKWELIKWELI


"Wenzetu alama yao ni kama kijiti hiki mnavyokiona!, achaneni nacho kitupeni, mpigieni kura Sioi alete maendeleo Arumeru." akasema Elirehema Kaaya ambaye naye 'alikula sahani moja' na Sioikwenye kura za maoni za CCM. Kushoto ni mratibu wa kampeni za CCM kitaifa Mwigulu

Nchemba akijibu tuhuma za chadema

Akizungumzia kuhusu CHADEMA kulalamikia Tume ya Uchaguzi kuwa haitawatendea haki kwenye uchaguzi huo, Mwigulu alisema, hata safu yao ya uonozi tangu Mwekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe hadi wabunge ikishika nafasi zote kwenye Tume hiyo CCM lazima itashinda uchaguzi wa Arumeru Mashariki utakaofanyika Aprili Mosi mwaka huu.
"Kwa Uchaguzi huu wa Arumeru Mashariki, hata Katibu Mkuu wa CHADEMA Dk. Wilborod Slaa awe Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Mbowe (Mweyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe) awe Mkurugenzi wa Uchaguzi, Zitto (Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Kabwe Zitto) awe Msimamizi Mkuu wa Uchaguzi  na wabunge wote  wa CHADEMA  wawe wasimamizi wa uchaguzi huo, halafu CCM tuweke mawakala tu, naapa kikwetu CCM itashinda", alisema Mwigulu.

Alisema malalamiko ya CHADEMA dhidi ya vyombo vitakavyosimamia uchaguzi huo ni woga wa kushindwa kwa sababu wanafahamu kuwa CCM imejiimarisha vya kutosha Arumeru Mashariki na italirejesha jimbo.